in

Tumia Muonekano Mweusi Kwenye Kivinjari cha Chrome (Android)

Sasa tumia sehemu mpya ya Dark Mode kwenye kivinjari cha Chrome Android

Tumia Muonekano Mweusi Kwenye Kivinjari cha Chrome (Android)

Kama wewe ni mtumiaji wa programu mbalimbali basi lazima utakuwa unajua kuwa Dark Mode au muonekano mweusi ni sehemu ya muhimu sana kwenye programu za siku hizi. Sehemu hii huweka muonekano mweusi kwenye programu husika na kuondoa rangi nyeupe na hivyo kufanya macho ya mtumiaji kuwa salama hasa anapokuwa anatumia programu hiyo wakati wa usiku.

Sasa siku za karibuni tumeona jinsi ya kuwasha muonekano huo mweusi kwenye kompyuta za Windows na Mac, lakini pia kidogo tuliangalia jinsi ya kuwasha sehemu hiyo kupitia programu na tovuti ya Tanzania Tech.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Kama kwa namna yoyote ulipitwa na makala hiyo basi labda nikufahamishe kwa ufupi kuwa unaweza kuwasha dark mode kwenye app ya Tanzania Tech kwa kubofya kwenye sehemu ya Mpangilio > Kisha chagua Soma Usiku. Kwenye tovuti ya Tanzania Tech bofya alama ya mwezi iliyopo juu upande wa kulia.

Tumia Muonekano Mweusi Kwenye Kivinjari cha Chrome (Android)

Sasa tuki achana na muonekano wa giza wa Tanzania Tech, sasa unaweza kuwasha muonekano huu wa giza kwenye kila tovuti unayotembelea kupitia kivinjari cha Google Chrome kwa mfumo wa Android. Ili kuweza kuwasha sehemu hii kwa sasa itabidi kutumia njia ya Flags ambayo nitakuonyesha hapo chini. Kama hujui kuhusu Flags basi unaweza kuangalia video hapo chini ya mambo ambayo ulikuwa huyajui kuhusu Google Chrome.

Sasa kama video hiyo ilivyo elekeza, ili kuwasha muonekano huu mweusi ingia kwenye kivinjari chako kisha bofya sehemu ya kuandika alafu andika chrome://flags.

Tumia Muonekano Mweusi Kwenye Kivinjari cha Chrome (Android)

Baada ya hapo utaona ukurasa mpya umefunguka wenye neno Experiments kwa chini. Kwenye sehemu ya kutafuta kwenye ukurasa huo (sehemu hiyo imeandikwa Search Flags) andika Dark Mode

Tumia Muonekano Mweusi Kwenye Kivinjari cha Chrome (Android)

Utaoa sehemu imeandikwa Android web contents dark mode, bofya kwenye sehemu iliyo andikwa Default kisha chagua Enabled.

Tumia Muonekano Mweusi Kwenye Kivinjari cha Chrome (Android)

Baada ya hapo bofya sehemu ya Relaunch itakayo tokea chini upande wa kulia. Baada ya hapo utaona kivinjari cha Chrome kimejifunga na kujifungua kisha ukingia kwenye sehemu ya kutafuta kitu mtandaoni utaona sasa ina muonekano wa rangi nyeusi.

Tumia Muonekano Mweusi Kwenye Kivinjari cha Chrome (Android)
Kama kwa namna yoyote hauto pendezwa na muonekano huo unaweza kurudia hatua hizo kisha bofya sehemu hiyo na weka default au unawea kubofya sehemu ya Reset all to default kisha funga kabisa kivinjari cha chrome na ufungue tena, sehemu hiyo kama inaonekana kwenye picha hapo chini ipo upande wa kulia juu.

Tumia Muonekano Mweusi Kwenye Kivinjari cha Chrome (Android)

Kama umefanikiwa kuwasha muonekano huo hebu tuambie maoni yako unaonaje muonekano huo na pia kama hujapenda muonekano huo unaweza pia kutuambia kupitia sehemu ya maoni hapo chini.

Tumia Muonekano Mweusi Kwenye Kivinjari cha Chrome (Android)
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.